ARUSHA NJOONI KATIKA TAMASHA LA UMWEMA : FINA AKYOO


 

 Mwimbaji wa nyimbo za injili nchini Tanzania Fina Akyo amesema  Tamasha la Uzinduzi wa Albamu yake Mpya ya UMWEMA  litakuwa na utafauti mkubwa tofauti na ilivyo zoeleka katika Matamasha Mengine.

 Fina ameyasema hayo Wakati  akizungumza na Method Charles katika kipindi cha Gospel Climax kinacho Tazamwa kupitia Youtube Channel ya Habari Maalum Tv.

 Amesema angeweza kufanya uzinduzi huo Mapema kabla ya mwezi wa tisa ila kwasababu ya tatizo la ugonjwa wa korona ilipelekea kukatisha  swala la Uzinduzi huo.

 Fina kyoo anaye fanya  Vizuri na Wimbo wake wa Umwema anatarajia kuzindua album yake aliyo itambulisha kwa Jina la Umwema Jumapili ijayo ya September 13, 2020  katika kanisa la mlima Sinai lililopo Arusha kisongo Ghorofani kwa  mchungaji Zakaria Malima

 Tamsha hili la Uzinduzi  litaanza Mapema Baada ya watu kutoka kanisani Majira ya saa saba mchana  na Kuendelea.

Aidha amewaomba Watu Arusha kufika katika Tamasha hilo la Uzinduzi wa Albamu ya Umwema  ambalo litashehene waimbaji mbalimbali kutoka Arusha  ambao wamekuwa wakitamba na Nyimbo mbalimbali kama Vile Janet Kahembe, Daniel Isingo, Vaileth Daniel na Wengine wengi. 

Hata hivyo Fina amesema katika uzinduzi huo Mungu ataonyesha utofauti wake hasa vile  atakavyo jitukuza kupitia nyimbo zake na utukufu wa Mungu kutawala 

 

No comments:

Post a Comment