TIMU ya Azam FC imejinadi kuwa tayari imeshapata dawa ya mechi za mikoani ili kwenda sambamba na Simba na Yanga kwenye Ligi Kuu Bara kufuatia msimu uliopita kutofanya vema.
Azam wamesema msimu uliopita walipoteza mechi nyingi mkoani, hivyo wameamua kubadili mfumo wa mazoezi ili kuendana na hali ya viwanja vya mikoani ambavyo vingi vinaelezwa havina ubora.
Timu hiyo katika msimu uliopita ndani ya Ligi Kuu Bara, ilimaliza nafasi ya tatu nyuma ya mabingwa, Simba na Yanga.
Akizungumza na Spoti Xtra, Ofisa Habari wa Azam FC, Thabit Zakaria ‘Zaka Zakazi’ amesema: “Tathimini iliyofanyika katika ripoti ya msimu uliopita jambo la msingi ambalo limeonekana ni utumiaji wa uwanja.
No comments:
Post a Comment