
Serikali kupitia wizara ya kilimo Imeombwa kutengeneza sera itakayo hamasisha wakulima wa mazao mbalimbali kulima na kuhifadhi mbegu za asili ili kuzitunza zisipotee katika ramani ya Kilimo.
Ombi hilo limetolewa na wadau wa kilimo mkoani Arusha katika maadhimisho ya siku ya Chakula Duniani maadhimisho yaliyo Ratibiwa na Mtandao wa Vikundi vya wakulima mkoani arusha (MVIWAARUSHA) ambayo yalifanyika mkoani Arusha.
Gabriel Mwalabwi ni Mwenyekiti wa Mtandao wa vikundi vya wakulima Ekenywa amesema kuwa mbegu za asili ni mbegu ambazo zilikuwa zikitumiwa na mababu na mabibi na kwa kipindi hicho hakukuwa na Magonjwa mbalimbali ukilinganisha na hivi sasa ambapo magonjwa kwa mimea yameongezeka.
"Mbegu za asili tangu zamani zilivyo kuwa zikitumika zilikuwa hazina Magonjwa zinapo kuwa shambani tofauti na hivi sasa ambapo kwenye mbegu za kisasa tunaona kumekuwa na magonjwa Mengi hivyo tunaomba serikali kupitia wizara ya afya waweze kuweka sera ambayo itasaidia kulinda mbegu hizi za asili" Gabriel Mwalabwi Mwenyekiti wa Mtandao wa Vikundi vya wakulima.
Juliana Simon ni Mkulima kutoka mkoani Arusha ambaye amekuwa akitumia mbegu za asili ambazo anasema kwa sehemu kubwa zimesahaulika kutunzwa huku akitolea mfano juu ya mbegu zilizo sahaulikaza Nyanya.
"Zamani kulikuwa na Nyanya ndogondogo ambazo walizita nyny mshenzi lakini pia kulikuwa na nyanya ambazo zilikuwa zinajiotea na zilikuwa zina kaa muda mrefu bila kuoza tofauti na hizi sasa ambapo nyanya zinakaa muda mfupi tu zimeoza'' Alisema Juliana Saimoni Mkulima ambaye amekuwa akitumia mbegu za asili.
Akitolea Majibu kuhusu utunzaji na Uhifadhi wa Mbegu za asili kwa upande wa serikali katika maadhimisho ya siku chakula Duniani afisa kilimo mkoa wa Arusha Rose Moses amesema serikali imekuwa ikiwashauli wakulima kutumia mbegu za asili kulingana na Jogrofia ya maeneo kwani kuna baadhi ya maeneo ambayo mvua zipo chini ya wastani na mbegu.
Mbegu za asili ni muhimu kwa sababu zinaweza kusaidia kuendeleza kilimo cha kiasili, ambacho hakitegemei mbegu za kisasa au kemikali nyingi. Pia, zinaweza kusaidia katika kuhifadhi uhai wa mimea na viumbe vinavyotegemea mimea hiyo.
Serikali na mashirika yasiyo ya kiserikali nchini Tanzania wanafanya juhudi za kuendeleza na kuhifadhi mbegu hizi, ikiwemo kuanzisha vituo vya kuhifadhia mbegu na kutoa elimu kwa wakulima kuhusu umuhimu wa kutumia mbegu za asili.
MBEGU ZA ASILI ZILINDWE ZISIPOTEZWA NA ONGEZEKO LA MBEGU ZA KISASA : MVIWAARUSHA
Licha ya uwepo wa soko kubwa la zao la korosho nje ya nchi, baadhi ya wadau wa zao la korosho wameiomba serikali kuangalia upya utaratibu wa upatikanaji wa vibali na tozo kwani ni kikwazo kwa wadau hao katika kuyafikia masoko hayo.
Hayo yamebainishwa kwenye kikao cha mwaka cha wadau wakilimo na jukwaa huru la wadau wa kilimo kilicholenga kujadili fursa mbalimbali ikiwemo fursa za masoko ambayo imeonekana kuwa changamoto kwa wakulima wengi wakiwemo wa zao la korosho.
Akifunga mafunzo hayo mkurugenzi mtendaji wa ANSAF , Honest Mseri amesema wamebaini kuwa ili wakulima waweze kuzalisha kwa tija na kuuza bidhaa zao nje ya nchi nguvu kubwa inatakiwa kutumika kuimarisha vyama vya akiba na mikopo kwa wakulima , wafugaji na uvuvi.
Serikali yaomba kuimarisha Vyama vya Wakulima, Mifugo na Uvuvi
Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania – TARI, imedhamiria kuondoa changamoto ya zao la ngano nchini, kutokana na mahitaji ya ngano yalivyo kwa sasa kwa mwaka, kuwa ni tani 1,000,000 na uzalishaji uliopo ni tani 100,000 sawa na upungufu wa tani 900,000.
Akiongea katika maonesho ya wakulima yanayoendelea mkoani Mbeya, Mratibu wa zao la ngano Kitaifa – TARI kituo cha Selian Arusha, Ismail Ngolida amesema hatua hiyo itasaidia kuondoa mzigo mkubwa na kutumia fedha nyingi za kigeni kuiagiza kutoka nje.
Amesema, “ifikapo mwaka 2030 kunahitajika kuwe na uzalishaji unaofikia tani 2500 za mbegu za awali ambazo hizi mbegu za awali zitaweza kuzalisha tani 50,000 za mbegu zilizothibitishwa ubora, Mbegu hizi sasa zinaweza kupandwa eneo linalozidi hekta 400,000 ambazo zinaweza kutupatia hayo mahitaji ya ngano.”
Hata hivyo, Ngolida ameongeza kuwa moja ya mikakati ambayo Serikali ilimejiwekea ni kuzalisha mbegu za kutosha pamoja na kuongeza maeneo ya uzalishaji wa ngano, ili ifikapo mwaka 2030 nchi iwe imejitosheleza kwa uzalishaji wa zao hilo muhimu nchini.
TARI YADHAMIRIA KUONDOA CHANGAMOTO ZAO LA NGANO
Mradi wa kilimo endelevu plus umezinduliwa Jijini Arusha ukiwa na lengo la kukuza kilimo na kuchochea mfumo wa upatikanaji wa chakula kwa wakulima.
Akizindua mradi huo Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. John Mongella amesema Mradi huo utasaidia Taifa kuwa na uzalishaji wa chakula cha kutosha utakaochangia jamii kuwa na Afya bora.
Mkurugenzi wa island of peace (IDP) Ayesiga Buberwa Hiza amesema mradi huo utachangia utunzaji wa mazingira kwa kutumia kilimo ikolojia.
Kwa upande wake Afisa Kilimo Mkoa Arusha Rosemary Masawe amewapongeza wadau walioanzisha mradi huo kwa kuleta fursa na manufaa kwa wakulima wadogo.
Mradi wa kilimo endelevu Arusha plus Utafanyika kwa miak mitatu (3) huku ikilenga Vijana, wanawake na wakulima wa Vijijini.
Pia Mradi utasaidia kuanzisha Bustani Mashuleni na Kutoa elimu Mashuleni juu ya lishe na uzalishaji wa mfumo wa Chakula endelevu mashuleni.
Inaelezwa kuwa Utekelezaji wa Mradi huo utaimarishwa na kusimamiwa kikamilifu na Island of peace (IDP), RECODA na MVIWARUSHA katika wilaya mbili za mkoa wa Arusha.
“KILIMO ENDELEVU ARUSHA PLUS” KULETA AHUEWENI KWA WAKULIMA WADOGOWADOGO
Sampuli za viwatilifu 1005 kati ya Sampuli 1025 nchini Tanzania zimekidhi vigezo vya kutumika kwa wakulima baada ya Mamlaka ya Afya ya mimea na viwatilifu Tanzania Plant Health and pesticides authority(TPHPA) kufanya utafiti na kujiridhisha kuanzia mwaka 2022 hadi 2023.
Akizungumza katika Maadhimisho ya Mimea Duniani Kaimu Mkurugenzi wa TPHPA Dkt. Joseph Ndunguru ni sampuli Ishirini Kati ya Sampuli 1025 za Viwatilifu ambazo zilibainika kuto kukidhi Vigezo.
Profesa Iringaa Kweka ni msimamizi wa Viwatilifu kutoka TPHPA amesema katika kuhakikisha kuwa mazo kutoka Tanzania Yanakubalika nje ya Nchi mamlaka imekuwa ikitumia maabara yenye Ithibati ili kupima Ubaora na Usama wa Chakula.
Aidha amesema Ithibati ya Maabara inasaidia kuleta maendeleo ya Kilimo nchini Tanzania na Kukuza Kipato kwa Ngazi ya Kaya
Maadhimisho ya Siku ya Mimea Dunia Hufanyika May 12 ambapo kwa mwaka huu Kauli mbiu inasema Mimea Yenye Afya Isaidia Kuondoa Njaa, Kupunguza Umasikini, Kutunza Mazingira na Kukuza maendeleo ya Uchumi.
TPHPA : VIWATILIFU 20 KATI 1025 HAVIJAKIDHI VIGEZO KWA MATUMIZI YA MKULIMA
Asasi isiyo kuwa ya Kiserikali ya (SEIDA) ambayo Imekuwa ikijihusisha na Uimarisha wa Masoko ya Ndani ya Mazao ya Maharage inatarajia kupunguza Uhaba wa upatikanaji wa Mbegu hizo kwa kuzalisha mbegu kwa njia ya Umwagiliaji.
Hayo yamesemwa na Afisa Mradi kutoka Asasi hiyo Wilberth Wanga katika Warsha ya mafunzo ya Siku moja ya jinsi ya kuongeza thamani katika zao la Maharage.
Aidha ameongeza kuwa wanajitahidi kama mradi kutoa mafunzo kwa upandaji wa maharage pasipo kutegemea mvua peke yake na kuwapatia mbegu kwa ajili ya kuanzia lengo likiwa ni kuzalisha mbegu kwa wingi.
Bitrice Msafiri ni Mkurugenzi wa Kampuni ya (Bivac) ambayo inayo Jihuhusisha na Utoaji Elimu Kuhusu jinsi ya Kuongeza Thamani katika zao la Maharage ametoa wito kwa serikali kuwa na idadi ya wakulima ili kufahamu uhitaji halisi wa mbegu kwa wakulima.
Pia kwa upande wake mmoja ya wakulima ambaye amewahi kunufaika na mradi huo wa uongezaji thamani katika Maharage amesema bado wanasubiri mbegu hizo ambazo zinatarajiwa kuzalishwa na shirika hilo ili kupunguza changamoto hiyo.
Asasi ya (SEIDA) inashirikiana na mfuko wa kuendeleza mifumo masoko (AMDT) katika kufanikisha Mradi wa Kuhamasisha soko la ndani la la zao la Maharage kwenye lishe ya chaku;la linalo lenga upatikaji wa lishe Linganifu.
Wataalamu wa kilimo wanasisitiza kuwa kuwa maharage ni zao muhimu nchini Tanzania na ni zao la pili kwa umuhimu baada ya mahindi hivyo linapaswakulimwa kwa muktadha wa kibiashara na sio kwaa ajili ya kukidhi mahitaji ya familia pekee kwa kuweka juhudi katika kusambaza aina mpya za Mbegu.
CHANZO CHA HABARI
Jina : Wilbert Wanga
Huduma :Afisa Mradi
Mahali : Simanjiro | Manyara
Kampuni : SEIDA
Contact : +255 622 78 37 51
+255 765 36 11 51