BLUE CROSS SOCIETY YAZINDUA KAMPENI NAJIVUNIA KUTO KUTUMIA MADAWA YA KULEVYA

 

 



 

Arusha

Shirika lisilo la Kiserikali  linajihusisha na  afya kwa kijana na jamaii  zuia madhara yatokanayo na Pombe na Madawa ya Kulevya Blue Cross Society Tanzania  Limezindua kampeni iitwayo najivunia kuto kutumia Madawa ya kulevya ili kuwasaidia vijana  katika shule za msingi na sekondari wasijiingize Katika matumizi ya madawa ya kulevya.

 

Akizungumza mara baada ya Kuzindua kampeni Hiyo Afisa  mradi kutoka Blue Cross Tanzania  Anna Panga katika shule ya msingi na Sekondari Ngarenaro mkoani arusha amesema kwa kutumia Kampeni vijana wamekuwa wakielewa Zaidi elimu ya afya kwa kijana na jamaii  zuia madhara yatokanayo na Pombe na Madawa ya Kulevya.

 

Eva Mringi ni makamu mkuu wa shule ya msingi Ngarenaro ambaye amebaini kuwa kampeni  nah ii itawasaidia wanafunzi kujitambua  na kuto kujiingiza katika matuizi ya madawa ya kulevya na badala yake kujikita katika masomo na kuongeza ufaulu.

 

Moja ya Muhanga  wa Madawa ya kulevya ambaye alitumia madawa ya kulevya  kwa miaka Zaidi ya Ishirini na Baadae Kuacha  amewaasa viijana kuacha kuacha tabia ya kujiingiza katika matumizi ya madawa ya kulevya  kwani inavuruga hatima ya maisha.

 

Nao baadhi ya Wanafunzi kutoka shule ya msingi Ngarenaro wamesema kampeni hiyo inaendelea kuwakumbusha  na kuwasidia kujikita Zaidi katika  masomo.

 

Tanzania ipo nafasi ya tano kwa idadi ya watumiaji wa bangi barani Afrika, inaongoza eneo la Afrika mashariki ikiwa na watu milioni 3.6 wanaotumia bangi ikifuatiwa na Kenya ambayo iko nafasi ya sita na watu milioni 3.3 na Uganda katika nafasi ya nane ikiwa na watumizi milioni 2.6.

No comments:

Post a Comment