Askofu Batenzi Awasili Arusha kwaajili ya Mikutano ya Pasaka



 
Image result for batenzi
Askofu mkuu wa kanisa la FPCT Tanzania amewasili  mkoani Arusha kwaajili ya Mikutano  ya Pasaka ambayo itakuwa ikifanyika  katika kanisa la FPCT  Kimahama .

Akizungumza na Blog hii  Makamo askofu mkuu wa mkoa wa Arusha Mchungaji  Muna  amesema Akofu Batenzi  atahudumia mikutano ya yote ya Pasaka ambayo itakuwa inafanyika  katika kanisa la kimahama.

Aidha kwa upande wake Askofu Batenzi  akielezea ripoti ya mkutano wa umoja wa makanisa  duniani ulio fanyika  NgurudotoMkoani Arusha  amesema ni vema makanisa  yakawa na umoja katika kueneza injili kwa watu wote.

Askofu Batenzi  ataongoza mikutano yote ya Pasaka  na baada ya pasaka kupita atarejea mkoani Daresalaam kwaajili ya shughuli mbalimbali za kikanisa.

No comments:

Post a Comment