Wakristo wametakiwa kuwa na Imani wanapo shiriki katika Mikutano na Makongamano Mbalimbali ili Mungu aweze Kuachilia Majibu.
Akizungumza katika Kipindi cha Top Ten ya Habari Maalum fm Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Cornerstone Christian Church Shilo Lililopo Mbauda Yohana John amesema Mungu amekuwa akishindwa kuachilia majibu kwa sababu ya Imani Haba.
Mchungaji yohana amebainisha Kuwa Imani ya Mtumishi haitoshi kuachilia Majibu ya Mungu kwa Mtu Mwenye Tatizo.
“Kuna Mwanamke Mmoja Ambaye alihudhuria katika Kongamano la Wanawake Lililokuwa Limeandaliwa na Kanisa la Cornerstone Christian Church Baada ya kushinikizwa na Jirani Yake, Mwanamke huyu alikuwa ametumia Gharama Kubwa kwa wataalamu mbalimbali ili aweze kupata Mtoto alikuja na Imani Kuwa Mungu atamsaidia Katika Mzigo Mzito ambao aliubeba kwa Miaka 10 tangu ameingia kwenye Ndoa na Mungu alimjibu”Alisema Mchungaji Yohana John.
Aidha amesema Baada ya Kufika katika Maombi aliombewa na Kuondoka na alirudi Baada ya Miezi Mitatu Kutoa Ushuhuda Kuhusu Mungu alicho kifanya Baada ya Kubeba Ujauzito na Kwa sasa amejifungua Yupo salama na Mtoto.
Amesema Imani ya Mtu ni jambo ambalo Limebeba Majibu kwa Mtu katika Kufikia Mafanikio juu ya Kile ambacho mtu anaomba au kuombewa.
Hata hivyo amewataka wakristo kuto Yumbishwa na Visaidizi ambavyo Vimekuwa Vikitumika katika Nyakati hizi ili Kupokea Uponyaji na Badala yake Kuendelea Kuilinda Imani.
CHANZO CHA HABARI
Jina : Pastor Yohana John
Huduma : Mchungaji
Mahali : Arusha | Mbauda
Kanisa : Connerstone Christian Church Shilo
Contact : +255 764 12 77 28
No comments:
Post a Comment