Mwimbaji Wa Nyimbo Za Injili Kutoka Kundi La Machalii Wa Yesu Na Reporter Wa Gospel Trax ya Clouds Fm kutoka Arusha Douglas Kyungay Maarufu kama Dolaa Amemvisha Pete ya Uchumba Rafiki yake wa Muda Mrefu Glory Mathayo.
Akizungumza Katika Kipindi Cha Gospel News ya Habari Maalum Fm Dolaa Amesema Glory Mathayo Ni Rafiki Yake Wa Muda Mrefu Ni Kama Imekuwa Mwanzo Wa Milele.
“Najisikia Furaha Maana Nirafiki Yangu Wa Muda Mrefu Lakini Pia Ni Mtu Wangu Wa Karibu Kwa Muda Mrefu Nikama Imekua Mwazo Wa Milele Nilifurahi Sana wakati Nimeshika Pete Na Kumfurahia Sana Mungu” Amesema Dolaa.
Aidha Amesema Kuwa Anategemea Kufunga Ndoa Yake Siku Za Karibuni “Mwaka Huu Huu Haitafika Mwezi Wa Nane Tutakua Tumefunga Ndoa Yetu” Amesema Dolaa.
Kuhusu Ndoa za Vija wengi kuwa katika Changamoto na Baadhi ya Vijana Kushindwa Kuhimili na Kudumu katika Ndoa Amesema Matarajio Yake Ni Makubwa Atakapoingia Kwenye Ndo ana Anaamini Mungu atamuuongoza.
”Namuomba Mungu Ndoa Yangu Idumu Kwasababu Kuna Changamoto Nyingi Kila Mtu Ana Lalamikia Ndoa Lakini Mimi Napenda Kujifuza Kwa Wazee Maana Wazee Wanasema Changamoto Zipo Na ni Sehemu Ya Kupanda na Kushuka Ni Vyema Kujishusha “Amesema Dolaa.
“ Tuendelee Kuombeane Ukiona Mtu Anachangamoto Muombee Maana Ukimuombea Na Wewe Unabarikiwa Hata Kama Hatuonani Chamsingi Tuombeane” Amesema Dolaa.
Hata Hivyo Amesema Hatakaa Asahau Hilo Tukio La Kumvisha Mchumba Wake Pete Maana Watu Wengi Walikua Na Furaha Hata Kama Hali Ya Hewa haikuwa Rafiki kwani Mvua Lakini Watu Wengi Walikuja Kwa Wakati Na Kusheherekea Kwa Furaha.
No comments:
Post a Comment