Kuelekeza ‘mishale’ kwenye majimbo ya ubunge yanayoshikiliwa na upinzani ni moja ya majukumu waliyopewa washindi wa nafasi za juu katika uongozi wa CCM wa mikoa.
Katika chaguzi hizo, waliokuwa wasimamizi, wagombea na baadaye waliofanikiwa kushinda, wamekuwa ‘wakilishana yamini’ ya kuendesha mkakati wa kurudisha majimbo na kata walizoshindwa kwenye Uchaguzi Mkuu wa 2015.
Lakini wakati CCM ikijipanga, Chadema imekejeli mikakati hiyo ikisema kazi hiyo itakuwa rahisi ikiwa chama hicho kitatekeleza ahadi iliyoahidi kwa wananchi ikiwamo kutoa Sh50 milioni kila kijiji na kutokujikita kueneza propaganda badala ya maendeleo.
Baadhi ya mikoa inayotolewa macho na CCM ni Mbeya, Iringa, Manyara, Arusha, Dar es Salaam ambayo upinzani ulishinda majimbo na kata nyingi iliyowafanya kuongoza halmashauri na majiji ikiwa ni mara ya kwanza tangu kuanza uchaguzi wa vyama vingi vya siasa mwaka 1995.
January Makamba aliyekuwa msimamizi mkuu wa uchaguzi wa viongozi wa CCM Mkoa wa Iringa aliwataka wajumbe wa mkutano huo kuchagua viongozi watakaokiwezesha chama hicho kurejesha Jimbo la Iringa Mjini linaloshikiliwa na Mchungaji Peter Msigwa wa Chadema.
“Leo tunahitimisha mchakato wa uchaguzi Iringa, tunakwenda kupata safu mpya ya uongozi...uchaguzi ni fursa ya kupata safu mpya, kujipanga na kujiimarisha,” alisema waziri hiyo wa nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais –Muungano na Mazingira.
Makamba ambaye pia ni Mbunge wa Bumbuli aliongeza, “Mwaka juzi tulipata fursa ya kuondoa vichaka hapa Iringa lakini ikashindikana, katika uchaguzi huu ninaomba mchague kwa kuzingatia kuwa ipo haja ya kuwapata viongozi watakaofanikisha hilo.”
Mwenyekiti mpya aliyechaguliwa, Albert Chalamila alisema chama hicho kimepoteza mwelekeo mkoani humo kutokana na baadhi ya wanachama kuendekeza majungu, ufitini na uongo.
Alisema jukumu lililoko mbele yake sasa ni kuwaleta pamoja wanachama ili waweze kurejesha heshima ya chama hicho ndani ya Mkoa wa Iringa ambayo kwa sasa imetoweka.
“Iringa leo imepoteza majimbo matatu; Iringa Mjini, Halmashauri ya Manispaa ya Iringa na kutokana na wingi wa kura wa Chadema wakapata mbunge wa viti maalumu… kazi iliyo mbele yetu kwa sasa ni kuhakikisha tunarejesha majimbo hayo CCM,” alisema Chalamila.
 
Kuelekeza ‘mishale’ kwenye majimbo ya ubunge yanayoshikiliwa na upinzani ni moja ya majukumu waliyopewa washindi wa nafasi za juu katika uongozi wa CCM wa mikoa.
Katika chaguzi hizo, waliokuwa wasimamizi, wagombea na baadaye waliofanikiwa kushinda, wamekuwa ‘wakilishana yamini’ ya kuendesha mkakati wa kurudisha majimbo na kata walizoshindwa kwenye Uchaguzi Mkuu wa 2015.
Lakini wakati CCM ikijipanga, Chadema imekejeli mikakati hiyo ikisema kazi hiyo itakuwa rahisi ikiwa chama hicho kitatekeleza ahadi iliyoahidi kwa wananchi ikiwamo kutoa Sh50 milioni kila kijiji na kutokujikita kueneza propaganda badala ya maendeleo.
Baadhi ya mikoa inayotolewa macho na CCM ni Mbeya, Iringa, Manyara, Arusha, Dar es Salaam ambayo upinzani ulishinda majimbo na kata nyingi iliyowafanya kuongoza halmashauri na majiji ikiwa ni mara ya kwanza tangu kuanza uchaguzi wa vyama vingi vya siasa mwaka 1995.
January Makamba aliyekuwa msimamizi mkuu wa uchaguzi wa viongozi wa CCM Mkoa wa Iringa aliwataka wajumbe wa mkutano huo kuchagua viongozi watakaokiwezesha chama hicho kurejesha Jimbo la Iringa Mjini linaloshikiliwa na Mchungaji Peter Msigwa wa Chadema.
“Leo tunahitimisha mchakato wa uchaguzi Iringa, tunakwenda kupata safu mpya ya uongozi...uchaguzi ni fursa ya kupata safu mpya, kujipanga na kujiimarisha,” alisema waziri hiyo wa nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais –Muungano na Mazingira.
Makamba ambaye pia ni Mbunge wa Bumbuli aliongeza, “Mwaka juzi tulipata fursa ya kuondoa vichaka hapa Iringa lakini ikashindikana, katika uchaguzi huu ninaomba mchague kwa kuzingatia kuwa ipo haja ya kuwapata viongozi watakaofanikisha hilo.”
Mwenyekiti mpya aliyechaguliwa, Albert Chalamila alisema chama hicho kimepoteza mwelekeo mkoani humo kutokana na baadhi ya wanachama kuendekeza majungu, ufitini na uongo.
Alisema jukumu lililoko mbele yake sasa ni kuwaleta pamoja wanachama ili waweze kurejesha heshima ya chama hicho ndani ya Mkoa wa Iringa ambayo kwa sasa imetoweka.
“Iringa leo imepoteza majimbo matatu; Iringa Mjini, Halmashauri ya Manispaa ya Iringa na kutokana na wingi wa kura wa Chadema wakapata mbunge wa viti maalumu… kazi iliyo mbele yetu kwa sasa ni kuhakikisha tunarejesha majimbo hayo CCM,” alisema Chalamila.

CCM WAELEKEZA MISHALE MAJIMBO YA UKAWA






 
 
Kuelekeza ‘mishale’ kwenye majimbo ya ubunge yanayoshikiliwa na upinzani ni moja ya majukumu waliyopewa washindi wa nafasi za juu katika uongozi wa CCM wa mikoa.
Katika chaguzi hizo, waliokuwa wasimamizi, wagombea na baadaye waliofanikiwa kushinda, wamekuwa ‘wakilishana yamini’ ya kuendesha mkakati wa kurudisha majimbo na kata walizoshindwa kwenye Uchaguzi Mkuu wa 2015.
Lakini wakati CCM ikijipanga, Chadema imekejeli mikakati hiyo ikisema kazi hiyo itakuwa rahisi ikiwa chama hicho kitatekeleza ahadi iliyoahidi kwa wananchi ikiwamo kutoa Sh50 milioni kila kijiji na kutokujikita kueneza propaganda badala ya maendeleo.
Baadhi ya mikoa inayotolewa macho na CCM ni Mbeya, Iringa, Manyara, Arusha, Dar es Salaam ambayo upinzani ulishinda majimbo na kata nyingi iliyowafanya kuongoza halmashauri na majiji ikiwa ni mara ya kwanza tangu kuanza uchaguzi wa vyama vingi vya siasa mwaka 1995.
January Makamba aliyekuwa msimamizi mkuu wa uchaguzi wa viongozi wa CCM Mkoa wa Iringa aliwataka wajumbe wa mkutano huo kuchagua viongozi watakaokiwezesha chama hicho kurejesha Jimbo la Iringa Mjini linaloshikiliwa na Mchungaji Peter Msigwa wa Chadema.
“Leo tunahitimisha mchakato wa uchaguzi Iringa, tunakwenda kupata safu mpya ya uongozi...uchaguzi ni fursa ya kupata safu mpya, kujipanga na kujiimarisha,” alisema waziri hiyo wa nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais –Muungano na Mazingira.
Makamba ambaye pia ni Mbunge wa Bumbuli aliongeza, “Mwaka juzi tulipata fursa ya kuondoa vichaka hapa Iringa lakini ikashindikana, katika uchaguzi huu ninaomba mchague kwa kuzingatia kuwa ipo haja ya kuwapata viongozi watakaofanikisha hilo.”
Mwenyekiti mpya aliyechaguliwa, Albert Chalamila alisema chama hicho kimepoteza mwelekeo mkoani humo kutokana na baadhi ya wanachama kuendekeza majungu, ufitini na uongo.
Alisema jukumu lililoko mbele yake sasa ni kuwaleta pamoja wanachama ili waweze kurejesha heshima ya chama hicho ndani ya Mkoa wa Iringa ambayo kwa sasa imetoweka.
“Iringa leo imepoteza majimbo matatu; Iringa Mjini, Halmashauri ya Manispaa ya Iringa na kutokana na wingi wa kura wa Chadema wakapata mbunge wa viti maalumu… kazi iliyo mbele yetu kwa sasa ni kuhakikisha tunarejesha majimbo hayo CCM,” alisema Chalamila.
 
Kuelekeza ‘mishale’ kwenye majimbo ya ubunge yanayoshikiliwa na upinzani ni moja ya majukumu waliyopewa washindi wa nafasi za juu katika uongozi wa CCM wa mikoa.
Katika chaguzi hizo, waliokuwa wasimamizi, wagombea na baadaye waliofanikiwa kushinda, wamekuwa ‘wakilishana yamini’ ya kuendesha mkakati wa kurudisha majimbo na kata walizoshindwa kwenye Uchaguzi Mkuu wa 2015.
Lakini wakati CCM ikijipanga, Chadema imekejeli mikakati hiyo ikisema kazi hiyo itakuwa rahisi ikiwa chama hicho kitatekeleza ahadi iliyoahidi kwa wananchi ikiwamo kutoa Sh50 milioni kila kijiji na kutokujikita kueneza propaganda badala ya maendeleo.
Baadhi ya mikoa inayotolewa macho na CCM ni Mbeya, Iringa, Manyara, Arusha, Dar es Salaam ambayo upinzani ulishinda majimbo na kata nyingi iliyowafanya kuongoza halmashauri na majiji ikiwa ni mara ya kwanza tangu kuanza uchaguzi wa vyama vingi vya siasa mwaka 1995.
January Makamba aliyekuwa msimamizi mkuu wa uchaguzi wa viongozi wa CCM Mkoa wa Iringa aliwataka wajumbe wa mkutano huo kuchagua viongozi watakaokiwezesha chama hicho kurejesha Jimbo la Iringa Mjini linaloshikiliwa na Mchungaji Peter Msigwa wa Chadema.
“Leo tunahitimisha mchakato wa uchaguzi Iringa, tunakwenda kupata safu mpya ya uongozi...uchaguzi ni fursa ya kupata safu mpya, kujipanga na kujiimarisha,” alisema waziri hiyo wa nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais –Muungano na Mazingira.
Makamba ambaye pia ni Mbunge wa Bumbuli aliongeza, “Mwaka juzi tulipata fursa ya kuondoa vichaka hapa Iringa lakini ikashindikana, katika uchaguzi huu ninaomba mchague kwa kuzingatia kuwa ipo haja ya kuwapata viongozi watakaofanikisha hilo.”
Mwenyekiti mpya aliyechaguliwa, Albert Chalamila alisema chama hicho kimepoteza mwelekeo mkoani humo kutokana na baadhi ya wanachama kuendekeza majungu, ufitini na uongo.
Alisema jukumu lililoko mbele yake sasa ni kuwaleta pamoja wanachama ili waweze kurejesha heshima ya chama hicho ndani ya Mkoa wa Iringa ambayo kwa sasa imetoweka.
“Iringa leo imepoteza majimbo matatu; Iringa Mjini, Halmashauri ya Manispaa ya Iringa na kutokana na wingi wa kura wa Chadema wakapata mbunge wa viti maalumu… kazi iliyo mbele yetu kwa sasa ni kuhakikisha tunarejesha majimbo hayo CCM,” alisema Chalamila.

No comments:

Post a Comment