Akiwasili nchini Ugiriki, chimbuko la demokrasia duniani, Papa Francis amesema "majawabu mepesi" yanayotolewa na wanasiasa wa mrengo mkali wa kulia ni janga kwa demokrasia na kutoa wito wa kuweko dhamira mpya ya pamoja ya kuhimiza mwelekeo sahihi.
Kiongozi huyo wa kiroho ameitumia hotuba yake mbele ya viongozi wa kisiasa na kitamaduni nchini Ugiriki kutoa tahadhari kwa Ulaya kuhusu vitisho vinavyolikabili bara hilo linapokuja suala la siasa za hamasa.
Amesema kushiriki kwa mataifa yote duniani ndiyo kunaweza kutatua masuala nyeti yanayoukabili ulimwengu ikiwemo kuyalinda mazingira, kupambana na janga la virusi vya corona na hata umasikini.
"Hapa ndiyo demokrasia ilizaliwa" alisema Papa Francis akimwambia rais wa Ugiriki Katerina Sakellaropoulou na kufafanua wasiwasi alio nao juu ya hatma ya demokrasia barani Ulaya.
"Siasa inahitaji hili, ili kuweka maslahi ya pamoja mbele badala ya maslahi binafsi" amesema Papa Francis na kukumbusha kuwa Ulaya na ulimwengu hauwezi kupuuza hali ya kuanguka kwa misingi ya demokrasia duniani.
No comments:
Post a Comment