Wakristo wametakiwa kuwa makini katika ulimwengu huu kwa kutojiingiza kwenye maisha ya dhambi na kumwacha mungu kwani elimu ya dunia hii haiwezi zidi elimu ya Mungu.
Rai hiyo imetolewa na Askofu zakayo sanare wa kanisa la Baptist jimbo la Arusha magharibi wakati akihubiri katika kanisa la Baptist olmotonyi mkoani Arusha akiwataka wakristo kumtegemea Mungu kwa kila jambo.
Amesemamkuwa Yesu kristo ana majibu ya maisha ya kila mtu na tusikate tama juu ya mapito tunayoyapitia badala yake tumtegemee Mungu nae atatusaidia
Amesema kuwa kuwa katika maisha tunayoishi kila mmoja anatakiwa kuwa mnyeyekevu kwa mwingine kutojiinua badala yake tuishi kama Mungu anavyotaka tuishi.
Pia amewataka wazazi kuwalea watoto katika misingi iliyobora kwa kuwafundisha kama biblia inavyotuelekeza .
No comments:
Post a Comment