Katika Kikao cha Bunge nchini Kosovo, wabunge wa upinzani wameingia na gesi za machozi bungeni.

Wabunge hao waliwasha gesi hizo na kuvuruga mkutano huo ambao ulikuwa ukitaka kupiga kura kuhusu mpango wa ugawaji wa mipaka na Montenegro.

Inaelezwa kuwa walifungulia gesi hizo mara mbili kwa nyakati tofauti pindi kura hiyo ilipotakiwa kuanza kupigwa. Ilibidi polisi waingie bungeni humo na kuwatoa wabunge hao wa upinzani huku wabunge wawili wakiwa wamejeruhiwa.

Wabunge walipua gesi za machozi Bungeni


 
Katika Kikao cha Bunge nchini Kosovo, wabunge wa upinzani wameingia na gesi za machozi bungeni.

Wabunge hao waliwasha gesi hizo na kuvuruga mkutano huo ambao ulikuwa ukitaka kupiga kura kuhusu mpango wa ugawaji wa mipaka na Montenegro.

Inaelezwa kuwa walifungulia gesi hizo mara mbili kwa nyakati tofauti pindi kura hiyo ilipotakiwa kuanza kupigwa. Ilibidi polisi waingie bungeni humo na kuwatoa wabunge hao wa upinzani huku wabunge wawili wakiwa wamejeruhiwa.

No comments:

Post a Comment