Serikali ya Nigeria imethibitisha kuwa wengi kati ya wanafunzi wa kike 110 waliokuwa wametekwa na kikundi cha Boko Haram zaidi ya mwezi mmoja uliopita wameachiwa Jumatano asubuhi.

Shirika la habari la AFP limeripoti kuwa wasichana hao waliletwa katika mji wa Dapchi ulioko upande wa Kaskazini mwa Nigeria wa Jimbo la Yobe baada ya wale waliokuwa wanawashikilia kuwarejesha katika msafara ulioandamana na magari 9.

Ripoti za vyombo vya habari zimesema wasichana watano kati ya hao walikufa wakati wakisafirishwa, lakini afisa wa serikali wa jimbo la Yobe amesema hili bado halijaweza kuthibitishwa.

Vyanzo vya habari nchini Nigeria vimetoa habari kuwa wakazi wa eneo la Dapchi walikuwa wanafurahia kuachiwa kwa watoto hao.

Boko Haram yawaachia huru wanafunzi wa kike Nigeria


Serikali ya Nigeria imethibitisha kuwa wengi kati ya wanafunzi wa kike 110 waliokuwa wametekwa na kikundi cha Boko Haram zaidi ya mwezi mmoja uliopita wameachiwa Jumatano asubuhi.

Shirika la habari la AFP limeripoti kuwa wasichana hao waliletwa katika mji wa Dapchi ulioko upande wa Kaskazini mwa Nigeria wa Jimbo la Yobe baada ya wale waliokuwa wanawashikilia kuwarejesha katika msafara ulioandamana na magari 9.

Ripoti za vyombo vya habari zimesema wasichana watano kati ya hao walikufa wakati wakisafirishwa, lakini afisa wa serikali wa jimbo la Yobe amesema hili bado halijaweza kuthibitishwa.

Vyanzo vya habari nchini Nigeria vimetoa habari kuwa wakazi wa eneo la Dapchi walikuwa wanafurahia kuachiwa kwa watoto hao.

No comments:

Post a Comment