Jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga  linawashikilia watu sita wakiwemo raia wanne wa China kwa kosa la kusafirisha na kuhifadhi mawe yanayosadikiwa kuwa na madini  kinyume cha sheria.

Kwa mujibu wa Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga, ACP Simon Haule watuhumiwa walikamatwa Disemba 6,2017 saa saba mchana katika kata ya Ibadakuli wilaya ya Shinyanga na askari wa usalama barabarani wakati wakikagua roli lenye namba za usajili T 209 AVH lililokuwa limebeba mawe hayo yaliyochongwa mfano wa virungu.
Kamanda Haule alisema baada ya kuwakamata wachina hao na madereva wao, walisema mawe hayo wanayapeleka kuyahifadhi kwenye kwenye kiwanda cha kutengeneza mafuta ya kula cha Jielong Tz Co . Ltd kilichopo mjini Shinyanga.
Raia wa China waliokamatwa ni Bai Tao 40, Chen Dunlu 33, Huanran Liu  na Jianhua Xiong na madereva wao wawili ambao ni Anwari Shabani na Joseph Kapoli.
Mmiliki wa mali hizo Huanran Liu amekiri kutokuwa na lesseni wala kibali cha kusafirisha mawe hayo na kudai yeye ni mtafiti wa madini na ameyahifadhi kwenye kiwanda hicho cha mafuta kwa muda tu

Polisi Shinyanga yakamata wachina wakiwa na mawe yanayodaiwa kuwa na madini

 
 
 Jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga  linawashikilia watu sita wakiwemo raia wanne wa China kwa kosa la kusafirisha na kuhifadhi mawe yanayosadikiwa kuwa na madini  kinyume cha sheria.

Kwa mujibu wa Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga, ACP Simon Haule watuhumiwa walikamatwa Disemba 6,2017 saa saba mchana katika kata ya Ibadakuli wilaya ya Shinyanga na askari wa usalama barabarani wakati wakikagua roli lenye namba za usajili T 209 AVH lililokuwa limebeba mawe hayo yaliyochongwa mfano wa virungu.
Kamanda Haule alisema baada ya kuwakamata wachina hao na madereva wao, walisema mawe hayo wanayapeleka kuyahifadhi kwenye kwenye kiwanda cha kutengeneza mafuta ya kula cha Jielong Tz Co . Ltd kilichopo mjini Shinyanga.
Raia wa China waliokamatwa ni Bai Tao 40, Chen Dunlu 33, Huanran Liu  na Jianhua Xiong na madereva wao wawili ambao ni Anwari Shabani na Joseph Kapoli.
Mmiliki wa mali hizo Huanran Liu amekiri kutokuwa na lesseni wala kibali cha kusafirisha mawe hayo na kudai yeye ni mtafiti wa madini na ameyahifadhi kwenye kiwanda hicho cha mafuta kwa muda tu

No comments:

Post a Comment