Imeelezwa kuwa Baadhi ya Mafundisho ambayo Yamesahaulika katika kanisa la leo ni Mafundisho ya Kufunga na Kuomba.
Hayo yameelezwa na Mchungaji Godliver Rugumamu wa Kanisa la Calvary Assemblies of God lililopo Murieth Nazareth Mkoani Arusha.
Mchungaji Godliver amebainisha kuwa uhaba wa mafundisho ya kufunga na kuomba umesababishwa na Kanisa kuelemewa na kundi kubwa la wachungaji tofauti tofauti hali ambayo inafanya kuwepo kwa tatizo hilo la Mafundisho.
“Kumekuwepo na Kundi kubwa la la wachungaji tofautitofauti ambalo limekuwa likipambana na Misingi ya Kubarikiwa badala ya kupambana na misingi ya Kweli ya Kubarikiwa ya Kanisa” Mchungaji Godliver.
Amesema kuna baadhi ya wakristo wa leo wanapitia katika Maisha na Bado wanashindwa kufahamu yanatokaje na badala yake wamekuwa wakidanganywa.
Anesia Kamara ni Mshirika katika kanisa la Calvary assemblies of God ambaye amebainisha kuwa mtu asipo funga na Kuomba anakufa kiroho na anaweza asipate Mambo Mazuri kwa wakati kwa sababu Maombi bila Kufanga yanakuwa hayana Uzito.
Hata hivyo kwa upande wake Mchungaji Msaidizi wa kanisa hilo Amoni Swai amesema Kufunga na Kuomba ni kuutiisha Mwili kwani Mwili huwa unataka Mambo yake na Roho Inahitaji Mambo ya Rohoni hali inayofanya kuwepo na Uzito katikakufanya Mapenzi ya Mwili.
CHANZO CHA HABARI
Mchhungaji : Mchungaji Godliver Rugumamu
Contact : +255754287258
Kanisa : Calvary Nazareth
No comments:
Post a Comment