Wakristo wametakiwa kuwa Chombo kipya katika Bwana ili Mungu aweze Kukuza na Kuimarifasha Ufalme wake Duniani.
Akizungumza katika Ibada ya Jumapili katika kanisa la Fpct Ngongongare Mkoani Arusha Mchungaji Kiongozi wa kanisa hilo Hosea Mbise amesema kuwa mkristo wa Leo anatakiwa kumruhusu Mungu amfanye Chombo Kipya.
Amesema Mkristo kufanyika Chombo Kipya ni kujisafisha na kujitakasa ili Mungu amtengeneza upya na aweze kumtumia katika Kazi yake.
Aidha amebainisha kuwa Mungu hatazamii Chombo Kingine Zaidi ya Kumtumia Binadamu ili kufikisha ujumbe na Taaarifa mbalimbali za Kimungu.
Ameongeza kuwa Mungu hawezi kuwekeza Kipawa au huduma Yoyote kama Chombo chake kitakuwa kichafu anataka kuwekeza kwa Mtu ambaye amejitakasa.
Baadhi ya Wakristo walio Hudhuria katika Ibada hiyo wamesema kuwa chombo kipya katika Maisha ya wokovu ni mchakato endelevu kwa Mkristo Yoyote Yule.
Kanisa la FPCT Ngongongare lipo Magharibi mwa Mkoa wa Arusha lina Zaidi ya washirika 500 huku likiwa kanisa Mama Mkoani Arusha ambalo limekuwa likiongozwa na Mchungaji Kiongozi Hosea Mbise.
CHANZO CHA HABARI
Jina : Mchungaji Hosea MbISE
No comments:
Post a Comment