Na Yusta Mbuya
Wanafunzi wa shule za secondari wakumbushwa kufanya kilicho wapeleka shule.
Akizungumza na Habari Maalum fm Mwenyekiti wa Unaweza Festival Bwana Elinaja Estomih Mwanga amesema wanahudumia watoto ambao wako katika kipindi cha ukuaji ilikuwasaidia kiroho,kiakili na kimwili itasaidia kutatua changamoto wanazo zipata waweze kutambua kuna watu wanaweza kuwasadia.
Bwana Elinaja ameongezea kwa kusema kuwa event hiyo itasaidia kuwakumbusha wanafunzi kwamba Mungu amewapa nafasi ya kuwa shuleni ni kwa makusudi maalum iliwaje kulitumikia kanisa ,nchi na familia zao zinufaike kwa maisha yao.
Amebainisha kuwa watakuwepo Watumishi mbalimbali watakao hudumu katika event hiyo kama vile Sarah Ndoshi,Elia Mwatondo,Machali wa Yesu,Nelly music,Mkufunzi kutoka katika Chuo cha Uhasibu na Dactary kutoka KCMC Moshi.
Hata hivyo amemaliza kwa kusema kuwa lengo la event hiyo ni kutengeneza watu wenye mtazamo chanya juu ya maisha na kusudi ambalo Mungu ameweka kwenya maisha yao watu ambao watakuwa na matokeo mazuri kwenye jamii bila kujali Dini,kabira na matabaka yao.
Name : Elinaja Estomih
Tittle : Founder of Unaweza Festival
Contact : o686442494
No comments:
Post a Comment