WAMETUFUNGA LAKINI WAKAPIME KUJUA AFYA ZAO VUKA INITIATIVE WAENDELE NA ZOEZI LA KUHAMASISHA VIJANA KUPIMA :

 





Bonanza la Mpira wa Miguu lenye lengo la Kupima afya lililokuwa linafanyika Namanga Mkoani Arusha limehitimishwa kwa Namnga Worriors FC Kuibuka Mabingwa Mbele ya Maasai Worriors  na kukabidhiwa Kombe lao.


Bonanza hilo lililo fadhiliwa na Shirika lisilo la Kiserikali la Vuka Initiative lililopo Mkoani Arusha lenye Lengo la kuhamasisha Vijana kupima afya, Kujitambua na Kuchukua hatua wanapo Bainika na Maambukizi ya Magonjwa Mbalimbali.


Akikabidhi Kombe Hilo Mgeni rasmi wa Mashindano hayo amewataka Vijana  kukumbuka kupima afya ikiwa ni njia ya Kujiweka Salama katika Maisha ya Kila siku.


Vero Ignatus  ni Mkurugenzi wa Vuka Initiative Mkoani Arusha ambapo amesema Bonanza lilianza Tarehe Sita Mwezi wa sita Kata ya Longido wilaya ya Longido Mkoani Arusha yenye Kauli Mbiu ya “Jali afya yako Pima Kwa Hiari” ikiwa na lengo la kuwa kumbusha Vijana na Jamii kwa Ujumla Kupima afya zao Kwa Hiari.


“Niwaase Vijana  Wenzangu Usiogope Kupima afya yako unapo pima afya yako  na kujigundua kuwa una maambukizi ina kuwa ni Rahisi wewe Kuanza Matibabu Mapema sio kwa maambukizi ya Ukimwi tu na Hata Magonjwa Mengine” Alisema Vero Ignatus Mkuruenzi wa Vuka Initiative.


Ignus Lwena Katibu wa Chama cha Mpira wa Miguu Wila ya Longido Amewashukuru Vuka Initiative na kampuni ya Kichina Inayojenga Mzani wa Kimokoa kwaletea Bonanza hilo na kuhamasisha vijana Kupima afya ili kutatua changamoto ya Muda Mrefu ya Vijana  wa Wilaya hiyo  Kuto kuwa na Mazoea ya Kupima Afya zao.


Hata hivyo kwa Upande wa Kapteni wa Timu ya Maasai Worriors ambao walikuwa washindi wa Pili katika Mchezo huo Baada ya Kufungwa na Namanga Worriors Wamesem a Licha ya Kuwa Wamefungwa na Kuchukuwa Kombe katika Bonanza Hilo wakapime ili kujua Afya Zao.


Vuka Initiave ni Shirika lisilo la Kiserikali ambalo limekuwa likijihusisha na Kupinga Ukatili na Kuhamasisha vijana kujikinga na Magonjwa mbalimbali ikiwemo  ya Kuambukiza na Yasiyo ya Kuambukiza.


 

 CHANZO CHA HABARI

Jina : Vuka Initiative

Mahali  : Arusha

Contact : +255714903131

No comments:

Post a Comment