Bonanza la Mpira wa Miguu lenye lengo la Kupima afya lililokuwa linafanyika Namanga Mkoani Arusha limehitimishwa kwa Namnga Worriors FC Kuibuka Mabingwa Mbele ya Maasai Worriors na kukabidhiwa Kombe lao.
Bonanza hilo lililo
fadhiliwa na Shirika lisilo la Kiserikali la Vuka Initiative lililopo Mkoani
Arusha lenye Lengo la kuhamasisha Vijana kupima afya, Kujitambua na Kuchukua
hatua wanapo Bainika na Maambukizi ya Magonjwa Mbalimbali.
Akikabidhi Kombe Hilo Mgeni
rasmi wa Mashindano hayo amewataka Vijana
kukumbuka kupima afya ikiwa ni njia ya Kujiweka Salama katika Maisha ya
Kila siku.
Vero Ignatus ni Mkurugenzi wa Vuka Initiative Mkoani Arusha
ambapo amesema Bonanza lilianza Tarehe Sita Mwezi wa sita Kata ya Longido
wilaya ya Longido Mkoani Arusha yenye Kauli Mbiu ya “Jali afya yako Pima Kwa
Hiari” ikiwa na lengo la kuwa kumbusha Vijana na Jamii kwa Ujumla Kupima afya
zao Kwa Hiari.
“Niwaase Vijana Wenzangu Usiogope Kupima afya yako unapo pima
afya yako na kujigundua kuwa una
maambukizi ina kuwa ni Rahisi wewe Kuanza Matibabu Mapema sio kwa maambukizi ya
Ukimwi tu na Hata Magonjwa Mengine” Alisema Vero Ignatus Mkuruenzi wa Vuka
Initiative.
Ignus Lwena Katibu wa
Chama cha Mpira wa Miguu Wila ya Longido Amewashukuru Vuka Initiative na
kampuni ya Kichina Inayojenga Mzani wa Kimokoa kwaletea Bonanza hilo na
kuhamasisha vijana Kupima afya ili kutatua changamoto ya Muda Mrefu ya
Vijana wa Wilaya hiyo Kuto kuwa na Mazoea ya Kupima Afya zao.
Hata hivyo kwa Upande wa
Kapteni wa Timu ya Maasai Worriors ambao walikuwa washindi wa Pili katika
Mchezo huo Baada ya Kufungwa na Namanga Worriors Wamesem a Licha ya Kuwa
Wamefungwa na Kuchukuwa Kombe katika Bonanza Hilo wakapime ili kujua Afya Zao.
Vuka Initiave ni Shirika
lisilo la Kiserikali ambalo limekuwa likijihusisha na Kupinga Ukatili na
Kuhamasisha vijana kujikinga na Magonjwa mbalimbali ikiwemo ya Kuambukiza na Yasiyo ya Kuambukiza.
Jina : Vuka Initiative
Mahali : Arusha
Contact : +255714903131
No comments:
Post a Comment