Na Method Charles
Mchungaji Kiongozi wa Kanisala EAGT
Mirerani Frank Msuya amehimiza wakristo kuamini katika Ushindi katika somo aliliofundisha kwenye Ibada ya Jumapili.
Akizungumza Katika kipindi cha Gospel Climax kinacho peperushwa kupitia Youtube Chanel ya Habari Maalum Media Mch Frank Msuya amesema amefundisha somo hilo kwa sababu mshindi ni yule mtu ambaye ana moyo wa kushinda kabla haja shinda hivyo aamini ya kwamba yeye ni mshindi.
Mchungaji Msuya amesema mtu ambaye anamuamini Kristo Yesu Yeye ni mshindi pia ametoa mfano wa mtu moja ambaye alikuwa anaitwa Samsoni kuwa alikuwa ni mshindi Kwasababu walimtoboa macho lakini Samsoni alikuwa bado ni mshindi kwakuwa alikuwa anania ya ushindi ndani yake.
Aidha naye Rehema Joseph Mshirika katika kanisa hilo amesema amejifunza kuwa yeye ni mshindi pia anawashauri watu wawe washindi kwasababu watashinda wakimwamini kristo ndani yao na wakiokoka.
Hata hivyo Tomas Edward Moja ya washirika katika Kanisa hilo amewataka watu kuamini katika ushindi na wajifunze kumtegemea Mungu kwa kila jambo na watashinda Mambo yote.
Kanisa la EAGT Mererani Mkoani Manyara ni moja ya kanisa ambalo limekuwa likihudumia Wakristo zaidi ya 100 kiroho na kuwaongoza njia ya Kwenda Mbinguni chini ya Mchungaji kiongozi wa Kanisa hilo Mchungaji Frank Msuya.
Chanzo cha Habari
KANISA : EAGT MERERANI
UJUMBE : MSHINDI
CONTACT : +255763990033
No comments:
Post a Comment